UPAMBANAJI WA KIJANA HUYU NI MFANO WA KUIGWA KWA VIJANA WENGINE
Kijana anaetambulika kwa jina la Johnson Kimaro mwenye umri wa miaka 28 ambae ameamua kujishughulisha na sanaa ya mitindo ya nywele yaani ususi iliyopo maeneo ya Nganza ambayo inamuingizia kipato katika kazi yake Pamoja na kuendesha familia yake licha ya kuwa anapitia changamoto mbalimbali kwenye kazi hiyo
LICHA YA UMAARUFU WAKE BADO KUNA CHANGAMOTO ZINAZOMKABILI KIJANA KIMARO
Licha ya ufanisi mkubwa anaoufanya Johnson katika kazi yake,pia kuna baadhi ya changamoto mbalimbali anazozipitia,ikiwemo ya kudharaulika katika jamii kwani watu wengi wanaamini kazi hiyo ni mahususi kwa wanawake tu kwani imezoeleka hivyo,pia mbali na hiyo jambo lingine ambalo linamletea shida ni kwa upande wa wasichana ambao hufanya nao kazi na kutaka kumpatia rushwa ya ngono(kimapenzi).
Aidha kwa upande mwingine Johnson aliwahasa vijana wenzake kwa kuamini wanachokifanya na kupambania ndoto zao ili wafikishe malengo yao licha ya changamoto zote ambazo watakuwa wanazipitia,kwani kwa kila jambo changamoto ni lazima lakini tu yawapasa kuwa wavumilivu,vicheko na madharau wao kwao yawapasa kuchukulia kama funzo na kuzidi kuweka bidii zaidi kwenye kazi zao.
Reviewed by Beatha
on
December 05, 2024
Rating:




No comments: